Mwenyekit wa UWT Taifa Ndugu Mary Chatanda amehutubia wananchi wa Kijiji cha Sambaru jioni ya Leo kwenye muendelezo wa ziara yake Wilayani Ikungi ambapo ametoa maelekezo kwa Waziri wa maji Mhe. Juma Aweso kufika kijijini hapo na kutatua kero ya maji kwa wananchi wa Kijiji hicho.
Aidha Chatanda akapata wasaha wa kuwasihi wananchi wa Ikungi kuwaapuuza wapinzani wanaokuja kupotosha juu ya utendaji kazi makini wa CCM chini ya Mwenyekit wake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu Samia Suluhu Hassan.
Ameyasema hayo tarehe 11 Agosti 2023.